Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Siku Kuu ya Wenyeji wa Asili kuadhimishwa kimataifa

Siku Kuu ya Wenyeji wa Asili kuadhimishwa kimataifa

UM na mashirika yake yamejumuika kuiheshimu \'Siku ya Kimataifa ya Watu wa Asili wa Dunia\' leo Ijumaa. Mada inayotiliwa mkazo katika taadhima za mwaka huu ni ile ya kukuza juhudi za upatanishi baina ya Mataifa wanachama na wenyeji raia wa asili. Taadhima rasmi za \'Siku ya Kimataifa kwa Wenyeji wa Asili\' hufanyika kila mwaka mnamo tarehe 09 Agosti, siku ambayo mwaka huu inaangukia Ijumamosi. ~