Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM unasisitiza mazeruzeru watekelezewe haki zao halali halan

UM unasisitiza mazeruzeru watekelezewe haki zao halali halan

Shirika la UM juu ya Miradi ya Maendeleo (UNDP) limenasihi kwenye ripoti iliotolewa karibuni ya kwamba ni muhimu kwa UM kujihusisha, kikamilifu, katika kugombania haki za mazeruzeru duniani. Wiki iliopita UNDP ilisimamia warsha maalumu katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (JKK) kuzingatia namna ya kuwasaidia mazeruzeru kujihudumia kimaisha, fungu la raia ambao kikawaida hukabiliwa na ubaguzi wa kila aina wa kijamii dhidi yao nchini.