Wanaotengua haki za ilimu wapewe adhabu, anasihi Villalobos
Vernor Munoz Villalobos, Mkariri Maalumu wa UM juu ya Haki za Kupata Ilimu ametoa taarifa maalumu Geneva inayopendekeza wale wanaoshambulia walimu, wanafunzi na maskuli wakamatwe na wapelekwe mahakamani kukabili haki na kuhukumiwa adhabu kali.