Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Majadiliano ya kina yameanza Ghana kusailia mkataba wa kudhibiti mabadiliko ya hali ya hewa duniani

Majadiliano ya kina yameanza Ghana kusailia mkataba wa kudhibiti mabadiliko ya hali ya hewa duniani

Wawakilishi 1,600 kutoka nchi wanachama 160 wamekusanyika hivi sasa kwenye mji wa Accra, Ghana kuhudhuria kikao cha wiki moja (21-27 Agosti 2008)kujadilia nidhamu za kuchukuliwa kipamoja kudhibiti bora tatizo la hewa chafu inayomwagwa angani, tatizo ambalo limethibitika kuwa ndio lenye kuharibu mazingira na kutifua mabadiliko ya kigeugeu ya hali ya hewa kimataifa. Mkutano umeandaliwa na Taasisi ya UM juu ya Mfumo wa Mkataba wa Kudhibiti Mabadiliko ya Hali ya Hewa Duniani (UNFCCC).