Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wajumbe wa Afrika wanashirikiana na UM Addis Ababa kuzingatia maendeleo ya wanawake

Wajumbe wa Afrika wanashirikiana na UM Addis Ababa kuzingatia maendeleo ya wanawake

Darzeni za wataalamu wa kutoka Wizara za Masuala ya Kijinsia na Maendeleo ya Wanawake wakijumuika pamoja na wawakilishi wa makundi ya kieneo na kutoka mashirika ya UM, na vile vile waandishi habari, wamekusanyika hii leo Addis Ababa, Ethiopia kuhudhuria mkutano wa siku mbili, ulioandaliwa bia na UM/UA, kusailia maendeleo ya wanawake, kijumla, na usawa wa kijinsia katika bara la Afrika. Majadiliano haya yatalenga zaidi juuya utekelezaji wa Sera za Kijinsiya za UA, mradi ambao unahitajia kutekelezwa na mataifa husika kuendeleza usawa wa kijinsiya na maendeleo ya wanawake Afrika.~~~