Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Guineau-Bissau ni mwenyeji wa mkutano wa UM kuzingatia hali Afrika Magharibi

Guineau-Bissau ni mwenyeji wa mkutano wa UM kuzingatia hali Afrika Magharibi

Mkutano wa kiwango cha juu wa siku mbili, unaohudhuriwa na Wajumbe Maalumu wa KM pamoja na wakuu wa mashirika yanayosimamia operesheni za ulinzi wa amani Afrika Magharibi, leo umeanzisha majadiliano katika Guinea-Bissau ambapo kunafanyika tathmini mpya juu ya hali, kijumla, na kusailia, hususan, taratibu za chaguzi zijazo katika mataifa ya Cote d’Ivoire, Guinea-Bissau na katika Jamhuri ya Guinea, vile vile kuzingatia udhibiti bora wa mipaka kwa sababu ya fununu za karibuni kwamba eneo la Afrika Magharibi siku hizi hutumiwa kusafirishia magendo ya madawa ya kulevya.