Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

BU linakutana kushauriana juu ya Burundi, Usomali na JKK

BU linakutana kushauriana juu ya Burundi, Usomali na JKK

Baraza la Usalama leo asubihi linazingatia hali katika Burundi kwenye kikao cha hadhara. Baada ya hapo Baraza litasailia kazi za Kamati ya Vikwazo dhidi ya JKK (DRC). Alasiri Baraza la Usalama linatarajiwa kuwa na mashauriano maalumu kuhusu maendeleo katika juhudi za kimataifa za kurudisha usalama na amani nchini Usomali, kikao ambacho pia kitahudhuriwa na Mjumbe Maalumu wa KM kwa Usomali, Ahmedou Ould-Abdallah.~