Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Benki kuu ya dunia inasema umasikini umekithiri ulimwenguni

Benki kuu ya dunia inasema umasikini umekithiri ulimwenguni

Benki Kuu ya Dunia imeonya ya kwamba umasikini umekithiri kwa wingi duniani kwa hivi sasa, kinyume na ilivyodhaniwa katika miaka ya nyuma. Benki Kuu imelazimika kurekibisha takwimu zake na sasa inakadiria watu bilioni 1.4, yaani robo moja ya idadi ya watu duniani, huishi kwenye hali mbaya ya umasikini, idadi ambayo ilikiuka makadirio ya nyuma ya watu milioni 985 walioashiriwa kuishi na pato la dola moja kwa siku. ~