Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM umekamilisha mafunzo ya polisi kwa Abyei, Sudan

UM umekamilisha mafunzo ya polisi kwa Abyei, Sudan

Shirika la UM juu ya Ulinzi wa Amani kwa Sudan Kusini (UNMIS) pamoja na Shirika la UM juu ya Miradi ya Maendeleo (UNDP) yamekamilisha mafunzo ya kwanza ya siku 10 kwa polisi wa Abyei, mji ambao umezongwa na vuguvugu la mvutano baina ya makundi ya kaskazini na kusini yalioshiriki kwenye mapigano ya miaka mingi, ya wenyewe kwa wenyewe katika Sudan.