Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WHO yahadharisha:ukosefu wa usawa unauwa 'halaiki ya umma' kimataifa

WHO yahadharisha:ukosefu wa usawa unauwa 'halaiki ya umma' kimataifa

Uchunguzi wa miaka mitatu wa Kamisheni juu ya Viashirio vya Afya ya Jamii, uliodhaminiwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) wiki hii umewasilisha matukio ya utafiti wao iliobainisha kwamba licha ya kuwa uchumi unaendelea kunyanyuka katika nchi kadha duniani, muongezeko huu wa utajiri wa taifa pekee hausaidii kusawazisha hali ya usawa katika huduma za afya ya umma, kwa ujumla.