Holmes anaelekea Ethiopia kutathminia hali ya ukame na njaa
John Holmes, Naibu KM juu ya Masuala ya Kiutu na Mshauri kuhusu Misaada ya Dharura ya UM anatarajiwa kuwasili Ethiopia Septemba mosi kushauriana na Serikali juu ya namna ya kuwasaidia kudhibiti tatizo la njaa liliofumka kwa sababu ya kutanda kwa ukame mbaya nchini humo.