KM ameanza ziara rasmi Uchina
KM wa UM Ban Ki-moon leo ameanza ziara rasmi ya siku tatu Uchina ambapo anatarajiwa kuzungumza na viongozi wa taifa hilo masuala kadha wa kadha juu ya uhusiano wa kimataifa, pamoja na umuhimu wa Uchina kutekeleza majukumu yake katika udhibiti bora wa athari za mabadiliko ya hali ya hewa duniani. ~