Holmes ainasihi Zimbabwe kuondoa vikwazo dhidi ya wagawaji misaada
Mshauri wa UM juu ya Misaada ya Dharura, John Holmes, ameiomba Serikali ya Zimbabwe kuondosha vikwazo dhidi ya mashirika yasio ya kiserikali yaliopo nchini humo, kwa sababu vikwazo hivyo vinaathiri hali za watu milioni 2 nchini humo wanaotegemea misaada ya kimataifa kumudu maisha.