Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Waathiriwa wa mafuriko Msumbiji wanahitaji suluhu ya kudumu, asema mtaalamu wa UM

Waathiriwa wa mafuriko Msumbiji wanahitaji suluhu ya kudumu, asema mtaalamu wa UM

Baada ya kukamilisha ziara ya uchunguzi nchini Msumbiji, Mjumbe wa KM juu ya Haki za Wahamiaji wa Ndani Waliong\'olewa Mastakimu, Walter Kaelin, alitoa mwito unaoitaka Serikali ya Msumbiji, pamoja na jamii ya kimataifa, kukuza juhudi za kuwapatia makazi na huduma nyengine za kuendeleza maisha ya kawaida wale watu walioharibiwa mali zao na mafuriko yaliojiri nchini humo miezi ya karibuni.