Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kundi la G-8 lakusanyika Ujapani kuzingatia maendeleo ulimwenguni

Kundi la G-8 lakusanyika Ujapani kuzingatia maendeleo ulimwenguni

Wakati viongozi wa Kundi la G-8 wanakusanyika katika kisiwa cha Ujapani kaskazini cha Hokkaido, kwenye Mkutano Mkuu wa mwaka, KM Ban Ki-moon, ambaye pia anahudhuria mkusanyiko huo, aliwaambia waandishi habari hii leo kwamba hatua za haraka zinatakikana kuchukuliwa na mataifa yenye utajiri wa viwandani, kutekeleza zile ahadi walizotoa siku za nyuma, za kuongeza kwa mara mbili zaidi misaada ya maendeleo kwa Afrika pale itakapofika 2010.