Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

G8 inalenga kupunguza hewa chafu kwa nusu katika 2050

G8 inalenga kupunguza hewa chafu kwa nusu katika 2050

Viongozi wa Kundi la G8, ambalo huwakilisha mataifa yenye maendeleo makubwa ya viwandani duniani, wameafikiana kupunguza kwa asilimia 50 umwagaji wa hewa chafu angani itakapofika 2050. Ahadi hiyo ilitolewa kwenye majadiliano yanayofanyika kwenye kisiwa cha Hokkaido, Ujapani. Maafikiano haya yanadaiwa yatasaidia udhibiti bora wa athari za mabadiliko ya hali ya hewa ulimwenguni.