Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Watalaamu wa UM/UU kuisaidia Philippines kudhibiti uharibifu wa sumu kutoka feri iliozama

Watalaamu wa UM/UU kuisaidia Philippines kudhibiti uharibifu wa sumu kutoka feri iliozama

Timu ya wataalamu wa UM na Umoja wa Ulaya (UU) hii leo wameelekea Philippines kuitika ombi la Serikali, ili kutathminia viwango vya sumu kali ya kemikali iliomwagika kutoka shehena ya mapipa ya dawa za kuua wadudu, yaliokuwa yamepakiwa kwenye ile feri iliozama karibu na Kisiwa cha Sibuyan, mnamo Juni 21 (2008), baada ya kupigwa na Kimbunga Fengshen.