Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Siku ya Kudhibiti Idadi ya Watu Duniani

Siku ya Kudhibiti Idadi ya Watu Duniani

Tarehe 11 Julai huadhimishwa kila mwaka na UM kuwa ni Siku ya Kudhibiti Idadi ya Watu Duniani. Risala ya KM Ban Ki-moon pamoja na Thoraya Ahmed Obaid, Mkurugenzi wa Shirika la UM juu ya Mfuko wa Kudhibiti Mifumko yaIdadi ya Watu (UNFPA) kuadhimisha siku hiyo imekumbusha tena kwamba lengo la 5 la MDGs la kupunguza vifo vya uzazi limezorota duniani na lipo nyuma ya maendeleo yote mengine ya milenia na linahitajia kurekibishwa haraka ili uzazi wa majira udhibitiwe vyema na kunusuru maisha ya mama na watoto kwenye nchi masikini. ~ ~~