Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

CITES inakutana Geneva kusailia biashara ya pembe na mbao adimu

CITES inakutana Geneva kusailia biashara ya pembe na mbao adimu

Mkutano wa UM wa kikao cha 57 cha Kamati Ndogo juu ya utekelezaji wa Mkataba wa Biashara ya Kimataifa kuhusu Udhibiti wa Aina za Wanyama na Mimea Pori Inayohatarishwa Kuangamia (CITES) unafanyika Geneva wiki hii, kuanzia tarehe 14 Julai hadi 18 kuzingatai ombi la Uchina kuruhusiwa kuagizishia tani 100 za pembe za ndovu kutoka Afrika, akiba ambayo imevumbikwa sasa hivi kwenye maghala ya nchi nne za Kusini ya Afrika.