Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Misitu ya dunia itafanyiwa ukaguzi kuinusuru na mabadiliko ya hali ya hewa

Misitu ya dunia itafanyiwa ukaguzi kuinusuru na mabadiliko ya hali ya hewa

Shirika la Chakula na Kilimo (FAO), likishirikiana na nchi wanachama na wadau wengineo kutoka jumuiya kadha wa kadha za kimataifa, wameafikiana kuanzisha upimaji wa hali za misitu iliopo kwenye sehemu zote za ardhi ya dunia yetu, kwa kutumia vifaa vinavyoendeshwa kutokea mbali.