Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM kutetea waathiriwa wa zilzala Uchina kupata misaada ziada ya kihali

UM kutetea waathiriwa wa zilzala Uchina kupata misaada ziada ya kihali

Khalid Malik, Ofisa Mkaazi anayehusika na huduma za dharura Uchina, ametangaza kutokea mjini Beijing ya kwamba UM umeanzisha kampeni maalumu ya kuchangisha msaada wa dola milioni 33.5 wa kuwahudumia waathiriwa wa zilzala ya nguvu iliyotukia Mei 12 katika jimbo la Sichuan, tetemeko ambalo liliuwa watu 70,000 na kujeruhi mamia elfu wengine, na pia kusababisha zaidi ya watu milioni tano kukosa makazi.