Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNMACA imefanikiwa kufyeka mabomu 38,000 yaliotegwa Afghanistan

UNMACA imefanikiwa kufyeka mabomu 38,000 yaliotegwa Afghanistan

Haider Reza, Mkurugenzi wa Taasisi ya Kufyeka Mabomu yaliotegwa ardhini Afghanistan (UNMACA) amearifu kwamba katika miezi sita iliopita kumepatikana mafanikio ya kutia moyo ambapo yaliondoshwa, kwa usalama, mabomu 38,000 yaliotegwa na kuenezwa kwenye sehemu kadha za Afghanistan. Idadi hiyo ya mabomu yaliofukuliwa ardhini na kuangamizwa inajumuisha asilimia 10 ya mabomu yote yaliofyekwa nchini humo katika miaka 18 iliopita.