Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wasomali waliopo Finland kusaidia maendeleo ya afya Usomali kaskazini

Wasomali waliopo Finland kusaidia maendeleo ya afya Usomali kaskazini

Tawi la Finland la Shirika la Kimataifa juu ya Wahamaji (IOM), likisaidiwa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Finland, wameanzisha mradi mpya ujulikanao kama mpango wa Uhamaji na Maendeleo kwa Afrika (MIDA). Mradi utawahusisha Wasomali wahudumia afya 22, walio wakazi wa Finland wataalamu ambao watapelekwa Usomali Kaskazini kufanya kazi, kwa muda, na kutumia ujuzi na uzoefu wao kunyanyua sekta ya afya kimaendeleo.