Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Holmes kuzuru Myanmar kufuatilia huduma za kiutu

Holmes kuzuru Myanmar kufuatilia huduma za kiutu

Mkuu wa UM anayehusika na misaada ya dharura, John Holmes amewasili Myanmar Ijumanne, kwa ziara ya siku tatu, kutathminia hali ya waathiriwa wa Kimbunga Nargis na maendeleo katika kufarajia misaada ya kiutu, pamoja na juhudi za Myanmar za kufufua tena huduma za kiuchumi na jamii. Baada ya kuwasili kwenye mji wa Yangon Holmes alipanda helikopta na kwenda moja kwa moja kwenye eneo la Delta la Ayeyarwardy, liliopo kusini, ambapo uharibifu mkubwa ulipofanyika mwezi Mei.mkulipotukia uharibifu mkubwa zaidi mwezi Mei kutokana na Kimbunga Nargis, tufani iliosababisha watu 138,000 ama kufariki au kupotea nchini. Shughuli za kufufua huduma za kiuchumi na jamii zinaendelea kukithiri, zikisimamiwa na mashirika kadha ya kimataifa yaliopo katika vituo sita vya Delta la Ayeyarwady. ~