Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kukamatwa kwa Karadzic kwasherehekewa na UM dhidi ya uhuru wa kupona adhabu

Kukamatwa kwa Karadzic kwasherehekewa na UM dhidi ya uhuru wa kupona adhabu

Mnamo Ijumatatu ya tarehe 21 Julai (2008) Radovan Karadzic, aliyekuwa Raisi wa Republika Srpska wakati wa vita katika Bosnia-Herzegovina, alishikwa na watu wa usalama wa Serbia. Karadzic alikamatwa baada ya kujificha kwa muda wa miaka 13 na kukwepa sheria yakimataifa iliomshitaki katika Julai 25, 1995 kuwa alihusika na mauaji ya halaiki dhidi ya watu wasio Waserb katika Bosni-Herzegovina, ikijumuisha WaBosnia walio Waislamu na Wacroat.

Sikiliza habari kamili kwenye idhaa ya mtandao.