Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Sudan na UM kutiliana sahihi maafikiano ya kukuza maendeleo nchini

Sudan na UM kutiliana sahihi maafikiano ya kukuza maendeleo nchini

Serikali ya Sudan leo imetiliana sahihi na mashirika 18 ya UM yaliopo nchini mkataba wa miaka minne, wenye dhamira ya kulisaidia taifa hilo katika huduma za ujenzi wa amani na kwenye shughuli za utawala, uamirishaji wa taratibu za kufuata sheria pamoja na huduma za kuzalisha ajira, kuimarisha elimu na afya ya jamii.