Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

OCHA imeripoti Wakongo 65,000 wafukuzwa Angola

OCHA imeripoti Wakongo 65,000 wafukuzwa Angola

Christophe Illemassene, Msemaji wa Shirika la UM juu ya Misaada ya Dharura (OCHA) katika JKK ameiambia Redio ya UM-Geneva kwamba wana taarifa iliothibitisha kuwa tangu Mei mwaka huu raia wa Kongo 65,000 walifukuzwa na kuondoshwa kutoka Angola, wingi wao wakiwa wale wahamiaji walioingia Angola bila sheria, wakitafuta ajira kwenye viwanda vya migodi.