Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNCTAD imewasilisha ripoti mpya ya biashara na maendeleo duniani

UNCTAD imewasilisha ripoti mpya ya biashara na maendeleo duniani

Shirika la UM juu ya Biashara na Maendeleo (UNCTAD) limewasilisha Geneva takwimu mpya kwa 2008 juu ya biashara ya kimataifa. Takwimu za UNCTAD zimethibitisha katika 2007 biashara baina ya nchi zinazoendelea ziliongezeka. Lakini ripoti pia ilitilia mkazo nchi ziliotawala kwenye soko la kimataifa, hasa kwenye shughuli za kusafirisha bidhaa nje na kwenye biashara za huduma zilikuwa ni mataifa yenye maendeleo ya viwandani. Asilimia 70 ya jumla ya pato la ulimwengu katika 2007 iliwakilishwa katika nchi zenye maendeleo ya viwandani licha ya kuwa idadi yao ni asilimia 15 ya umma wa kimataifa.