Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mshauri wa KM anazuru eneo la Sahel kutathminia hali

Mshauri wa KM anazuru eneo la Sahel kutathminia hali

Jan Egeland, Mshauri Maalumu wa KM ameanza ziara ya siku tano kuyatembelea mataifa ya Sahel mapema wiki hii. Ijumatatu alikuwepo Burkina Faso ambapo alinakiliwa akisema kwamba eneo la Sahel ni kama ‘ardhi chimbuko’ yenye kufukuta mabadiliko ya hali ya hewa yanayosababisha mizozo aina kwa aina, hali ambayo inahitajia kudhibitiwa haraka, aliongeza kusema.