Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

KM atathminia mzozo wa chakula

KM atathminia mzozo wa chakula

KM Ban Ki-moon, kabla ya kuondoka Roma, alikutana na waandishi habari ambapo alinasihi kwamba walimwengu wamekabiliwa na uamuzi mmoja pekee katika kuutatua mgogoro wa chakula duniani. Uamuzi huo ni ule utakaohakikisha tunafanikiwa kulimudu tatizo la chakula kipamoja, ili kuepukana na maafa ya adui njaa.