Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Usawa wa Kijinsiya Makazini unasisitizwa na ILO

Usawa wa Kijinsiya Makazini unasisitizwa na ILO

Shirika la UM juu ya Haki za Wafanyakazi Duniani (ILO) limeanzisha kampeni mpya ya kimataifa itakayoendelezwa kwa muda wa mwaka mmoja, iliokusudiwa kuangaza umuhimu wa kuwa na usawa wa kijinsia katika mifumo ya kazi na ajira. Kadhia hii inalingana na mapendekezo ya Ajenda ya Kazi Stahifu, ambayo inajumuisha mada 12 zinazotumiwa kupitia athari za mifumo ya kazi na ajira miongoni mwa wafanyakazi wanaume na wanawake, na kufafanua kama haki zao hutekelezwa kwa usawa. ~~