Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mashambulio ya raia Kivu Kaskazini kulaaniwa na UNHCR

Mashambulio ya raia Kivu Kaskazini kulaaniwa na UNHCR

Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) limelaani mashambulio yaliotukia kwenye kambi ya muda iliopo eneo la mashariki katika JKK ambapo iliripotiwa watu karibu tisa waliuawa, wakiwemo watoto wadogo wawili, na korja ya watu wengine kujeruhiwa. UNHCR pamoja na mashirika yanayohudunmia misaada ya kiutu yameamua hivi sasa kusitisha operesheni zao na kuhamisha wafanyakazi, kwa muda, kutoka eneo la Kivu Kaskazini, kilomita 70 kaskazini ya mji wa Goma.~