Mkutano wa Kudhibiti Mzozo wa Chakula Duniani umeahidi misaada maridhawa kwa mafukara muhitaji wa kimataifa
Mkutano Mkuu wa UM juu ya Udhibiti Bora wa Akiba ya Chakula Duniani uliofanyika mjini Roma, Utaliana ulikhitimishwa Alkhamisi baada ya siku tatu ya majadiliano makali miongoni mwa Mataifa Wanachama. Ripoti ya mwisho iliopitishwa iliahidi jamii ya kimataifa itajumuika kipamoja "kukomesha njaa pote ulimwenguni na kudhaminia kupata chakula ule umma muhitaji bilioni moja, hivi sasa na katika miaka ijayo." ~