Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Upungufu wa fedha kuilazimisha WFP kupunguza shughuli Sudan

Upungufu wa fedha kuilazimisha WFP kupunguza shughuli Sudan

Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limeripoti kwamba litalazimika kupunguza huduma zake za anga, zinazotumiwa kugawa misaada ya chakula kwa umma muhitaji katika eneo la mgogoro la Darfur, na kwenye sehemu nyengine zilizotawanyika masafa kadha wa kadha nchini Sudan.