Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mtaalamu wa UM anakhofia athari za sheria mpya dhidi ya ugaidi Uingereza

Mtaalamu wa UM anakhofia athari za sheria mpya dhidi ya ugaidi Uingereza

Martin Scheinin, Mkariri Maalumu anayehusika na utekelezaji wa haki za binadamu kwenye mazingira ya ugaidi, ametoa taarifa maalumu, hii leo, yenye kuonya kwamba pindi Bunge la Uingereza litaamua mnamo Juni 11 kupitisha Mswada wa Kupiga Vita Ugaidi, anakhofia uamuzi huo utaathiri zile juhudi za kutekeleza haki za kimsingi, kimataifa, ikimaanisha nchi nyengine nazo pia zitataka kuigiza, na kuhalalisha sheria hiyo kwenye vyombo vyao vya sheria.