Mkutano wa UM kukabiliana na UKIMWI wakaribia kumaliza mijadala
Mkutano wa Hadhi ya Juu wa UM Kukabiliana na UKIMWI unatarajiwa kukamilisha mijadala yake baadaye Ijumatano. Ijumanne KM Ban Ki-moon alifungua Mkutano kwenye ukumbi wa Baraza Kuu, na alidhihirisha kwenye risala yake kupatikana mafanikio ya kutia moyo hivi karibuni dhidi ya janga la UKIMWI, na alitoa mfano wa maendeleo kwenye juhudi za kuawapatia wanawake na watoto huduma za afya kinga.