Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WFP yaihimiza jamii ya kimataifa kufadhilia manowari dhidi ya uharamia Usomali

WFP yaihimiza jamii ya kimataifa kufadhilia manowari dhidi ya uharamia Usomali

Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limetoa ombi maalumu Alkhamisi linayoyataka yale mataifa yenye kumiliki majeshi makuu ya majini, kuisaidia UM kwa kuipatia manowari zao ili kulinda meli zinazochukua shehena ya chakula inayopelekwa Usomali, bidhaa ambayo inatakikana kukidhi mahitaji ya dharura kwa watu muhitaji milioni 2 watahatarishwa na tatizo maututi la njaa na utapia mlo pita watanyimwa posho hiyo.