Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

BU lasailia Zimbabwe kabla ya ziara ya Mjumbe wa KM

BU lasailia Zimbabwe kabla ya ziara ya Mjumbe wa KM

Baraza la Usalama (BU) leo limefanyisha kikao cha faragha kusailia tatizo la kiutu lilioselelea karibuni nchini Zimbabwe. Kikao hiki kinafanyika kabla ya KM Mdogo juu ya Masuala ya Kisiasa, Haile Menkerios hajaelekea Zimbabwe wiki ijayo, ambapo anatazamiwa kushauriana na viongozi husika kadha juu ya hali ya kisiasa, kwa ujumla, na vile vile kuzungumzia nawo kuhusu duru ya pili ya uchaguzi ujao wa uraisi utakaofanyika tarehe 27 Juni.

Haile Menkerios atazuru Zimbabwe kuanzia tarehe 16 hadi 20 Juni (2008).