Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Arbour kukaribisha uamuzi wa Mahakama Kuu ya Marekani kuhusu wafungwa wa Guantanamo

Arbour kukaribisha uamuzi wa Mahakama Kuu ya Marekani kuhusu wafungwa wa Guantanamo

Kamishna Mkuu wa UM juu ya Haki za Binadamu, Louise Arbour ameripotiwa kukaribisha kwa ridhaa kuu uamuzi uliotolewa Alkhamisi na Mahakama Kuu ya Marekani kuhusu ile kesi ijulikanayo kama Kesi ya Boumediene dhidi ya Bush, uamuzi ambao uliidhinisha kwamba watuhumiwa wa kigeni waliowekwa kizuizini na Serikali ya Marekani, bila ya idhini ya mahakama, kwenye zile jela ziliopo katika Ghuba ya Guantanamo, Cuba kuwa nawo pia wana haki halali ya kufikishwa kwenye mahakama za kiraia kujitetea na mashitaka dhidi yao.