Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mikutano ya Baraza la Usalama

Mikutano ya Baraza la Usalama

Baraza la Usalama asubuhi lilikutana kwenye kikao cha hadhara kusikiliza ripoti juu ya matokeo ya ziara ya karibuni ya tume ya Baraza ambayo ilitembelea Djibouti, Sudan, Chad, JKK na Cote d’Ivoire. Wawakilishi wa Kudumu wa Afrika Kusini na Uingereza walizungumzia kuhusu ziara ya ujumbe wa Baraza la Usalama katika Djibouti - kuzungumzia Usomali - na juu ya Sudan. Mjumbe wa Kudumu wa Ufaransa aliripoti kuhusu safari yao katika Chad na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo; na Balozi wa Burkina Faso, alityeipatia Baraza taarifa kuhusu Cote d\'Ivoire.