Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mfanyakazi wa UNHCR Usomali ametekwa nyara

Mfanyakazi wa UNHCR Usomali ametekwa nyara

Mfanyakazi mzalendo wa Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) nchini Usomali, Hassan Mohamed Ali, alitekwa nyara Ijumapili usiku kutoka nyumbani kwake, katika vitongoji vya mji mkuu wa Mogadishu na kundi la watu wenye silaha wasiotambulikana ambao walimchukua kwenye eneo lisiojulikana. Kwenye taarifa iliotolewa juu ya tukio hilo, UNHCR ilisema sababu za kutoroshwa kwa mfanyakzi wao huyo nazo pia hazijulikani.