Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Darfur inakabiliwa na janga la kiutu "timilifu", mashirika ya UM yaonya

Darfur inakabiliwa na janga la kiutu "timilifu", mashirika ya UM yaonya

Mashirika ya UM yaliopo kwenye eneo la Sudan magharibi la Darfur limetahadharisha kwenye taarifa iliotolewa ya pamoja kwamba hali iliojiri Darfur sasa hivi inaelekea kuzusha "dhoruba timilifu" ya matatizo ya kiutu, hususan yale matatizo yanayoambatana na upungufu wa chakula, halia ambayo imekorogwa zaidi kwa sababu ya kuongezeka kwa fujo na vurugu kieneo, na pia kufurika kwa kambi za umma uliong\'olewa makwao, ikichanganyika na mavuno haba katika mwaka huu.

Sikiliza ripoti kamili kwenye idhaa ya mtandao.