Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hali ya kisiasa Zimbabwe yapewa usikizi mkubwa na BU na KM

Hali ya kisiasa Zimbabwe yapewa usikizi mkubwa na BU na KM

Alasiri Baraza la Usalama lilikutana, kwenye kikao cha hadhara/faragha, kujadilia hali halisi ya kisiasa nchini Zimbabwe kufuatia uamuzi wa Morgan Tsvangirai, wa chama cha upinzani cha MDC, kujitoa kugombania uchaguzi wa urais ambao unatarajiwa kufanyika nchini mwisho wa wiki. KM wa UM, Ban Ki-moon, katika risala yake kuhusu suala hili, alioitoa kwa kupitia Msemaji wake, alisema anakhofia kitendo cha kiongozi wa MDC kujitoa kwenye uchaguzi kinatia "wasiwasi wa kina" na hakiashirii mema kwa mfumo wa demokrasia katika Zimbabwe.