Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNHCR inashinikiza mfanyakazi aliotekwa nyara Usomali aachiwe

UNHCR inashinikiza mfanyakazi aliotekwa nyara Usomali aachiwe

Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) limeripoti kuwa linaendelea kushinikiza, kwa sauti kuu, aachiwe huru yule mfanyakazi wao, Hassan Mohammed Ali, ambaye alitekwa nyara Ijumamosi iliopita kutoka nyumbani kwake katika mji wa Afgooye, kilomita 30 kutoka Mogadishu, na watu wasiojulikana. Kwa mujibu wa UNHCR mateka Ali aliweza kuzungumza kwa simu na aila yake Ijumapili usiku na alisema hali yake ni nzuri; lakini taarifa nyengine ziada yoyote kuhusu mahali alipo na utambulisho wa makundi yaliomtorosha haijulikani. ~