Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mwendesha Mashtaka wa ICC anasihi Lubanga asiachiwe

Mwendesha Mashtaka wa ICC anasihi Lubanga asiachiwe

Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa juu ya Makosa ya Jinai ya Halaiki (ICC) ametoa mwito maakumu unaowanasihi majaji wa korti hiyo kutomwachia mtuhumiwa wa kwanza wa mahakama, Thomas Lubanga aliyekuwa kiongozi wa majeshi ya mgambo katika JKK (DRC). Majaji wa Mahakama ya ICC wanazingatia kumwachia Lubanga kwa sababu ushahidi uliowakilishwa kwenye kesi yake ulikuwa na kasoro kisheria, dhidi yake. Miongoni mwa mashtaka aliotuhumiwa Lubanga ni lile kosa la kuwashirikisha watoto chini ya umri wa miaka 15 kwenye shughuli za vita na mapigano, katika eneo la mamshariki la Ituri, katika JKK. Mtuhumiwa amekataa makosa.~