Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wapatanishi wa UM/UA kwa Darfur waripoti mbele ya BU juu ya hali ya amani kieneo

Wapatanishi wa UM/UA kwa Darfur waripoti mbele ya BU juu ya hali ya amani kieneo

Wapatanishi wa UM na UA juu ya Darfur, yaani Jan Eliasson na Salim Ahmed Salim wamewasilisha ripoti zao mbele ya Baraza la Usalama kuhusu hali ya usalama na amani kwenye jimbo hili la mgogoro la Sudan magharibi. Mpatanishi wa UM Eliasson alisema kwenye risala yake kwamba yeye na Mpatanishi wa AU Salim wamependekeza kwa KM ateuliwe Mjumbe Maalumu juu ya Darfur, atakayekuwa na makao yake Khartoum, Sudan kushughulikia suala hilo, na wao wapo tayari kumsaidia mwakilishi huyo kwa kila njia kuleta amani kwenye jimbo la mgogoro.