Mkuu wa Idara ya Usalama ya UM Kajiuzulu

Mkuu wa Idara ya Usalama ya UM Kajiuzulu

David Veness, KM Mdogo anayehusika na Masuala ya Ulinzi na Usalama wa UM amemuarifu KM kwamba ameamua kujiuzulu, kwa khiyari, kwa sababu anaamini ilivyokuwa yeye ndio mwenye dhamana ya shughuli za Idara ya Usalama, ambayo ilishindwa kudhibiti hifadhi bora ya majengo ya UM mjini Algiers na kuashiria uwezekano wa kushambuliwa, aliwajibika kuwacha madaraka baada ya shambulio maututi la kigaidi kwenye majengo ya UM Algiers mnamo Disemba 2007.