Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM inasema wanawake wanahitajia kinga imara dhidi ya mateso

UM inasema wanawake wanahitajia kinga imara dhidi ya mateso

Taasisi za UM zinazoshughulikia juhudi za kimataifa za kukomesha mateso na kusaidia waathiriwa wa janga hili, zimetoa taarifa muhimu yenye kusisitiza kwamba walimwengu bado watahitajia kuchangisha bidii zao kwa wingi zaidi ili kufanikiwa "kuwapatia kinga na hifadhi madhubuti kila mwanadamu mstahiki dhidi ya mateso" licha ya kuwepo ulimwenguni kwa vyombo kadha wa kadha vya sheria ya kimataifa vinavyoharamisha janga hilo.