Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Nowak ainasihi Zimbabwe kusitisha mateso na fujo

Nowak ainasihi Zimbabwe kusitisha mateso na fujo

Manfred Nowak, Mkariri Maalumu wa UM juu ya Masuala ya Mateso na Vitendo Katili vya Kuadhibu na Kudhalilisha Utu ametoa mwito kwa Serikali ya Zimbabwe na jumuiya ya kimataifa wajumuike kipamoja, kidharura, kufanya kila wawezalo kusitisha haraka fujo na vitendo vya mateso nchini humo dhidi ya raia.