Nchi wanachama zahimizwa kuidhinisha mkataba dhidi ya mateso
Tarehe ya leo, Juni 26, inaheshimiwa kuwa Siku ya Kimataifa ya Ushikamano na Waathiriwa wa Mateso, siku ambayo KM aliitumia kutoa mwito unayoyahimiza Mataifa Wanachama wa UM kuidhinisha haraka Mkataba dhidi ya Mateso, na pia kuridhia Itifaki ya Khiyari ya Mkataba huo ambao hujumuisha pendekezo la kuchunguza, bila ya vizuizi, vituo vya kufungia watu vya kitaifa na kimataifa, ili kutathminia utekelezaji wa haki za wafungwa. ~